Kuwasili kwa kidato cha kwanza Hapo tarehe 4 Januari 2015 wanafunzi wapya wa kidato cha kwanza waliwasili hapa shuleni wakisindikizwa na wazazi, walezi, jamaa na marafiki, ili kuja kuanza hatua nyingine ya maisha. Uongozi wa shule uliwakaribisha na kuwaomba waanze maisha mapya kwa furaha na upendo, wakijua kwamba maisha yana mengi, hivyo huzuni za kuachana na wazazi wao zitazaa matunda hapo baadaye ya kupata Elimu na Malezi bora. Tuanawatakia wanafunzi wote maisha mema katika Shule yetu. |
Image |